Tanzania Forest Services (TFS) Agency

Ecotourism Destinations

Explore Life in Nature

Ecotourism Destinations
  • Home
  • About Us
    • Overview
    • Mission and Vission
    • Climate Conditions
    • Terms and Conditions
    • Frequently Asked Questions
    • Related Links
  • Destinations
    • Ecotourism Sites
    • Mangroove/Lakes/Beaches
    • Cultural & Heritage Sites
    • Api Tourism Sites
  • Activities
    • Mountain Climbing
    • Bird Watching
    • Cultural Tourism
    • Mountain Biking
    • Cultural Activities
    • Sundowners
    • Night Walk
    • Swimming
    • Forest Hiking
    • Research and Educational
    • Photographic Tourism
    • Butterfly Trailing
    • Camping and Picnicking
    • Adventure Safari
    • Sport Fishing
    • Canoeing
    • Historical Site Visits
    • Game Viewing
    • Walking Safari
    • Local brew Tasting
    • Worshiping Seclusion
    • Filming
    • Kayaking
    • Boat Excursion
    • Forest Walk
    • Acclimatization
    • Forest Drive Tour
    • Forest Trail Run
    • Forest Biking Trails
    • Forest Motor Cross
    • Recreation
  • Resources
    • Fees and Charges
    • Publications
    • Bronchures
    • Related Links
    • Photo Gallery
    • Videos
  • Newsroom
    • News and Events
    • Speeches
  • Plan Your Trip
    • Airline Flying to Tanzania
    • Bus Itinerary
    • Tour Operators
    • Accomodations
    • Exchange Rates
    • Entry Requirements
  • Contact Us
    • Head Office
    • Tourism Sites
  • You are here:
  • Home
  • Newsroom
  • TFS yapiga hatua kubwa katika uhifadhi wa misitu, ukuzaji utalii Tanzania

TFS yapiga hatua kubwa katika uhifadhi wa misitu, ukuzaji utalii Tanzania

  • Posted
  • by Admin
  • News and Events
  • 0

Utalii ni moja ya sekta nyeti zinazotegemewa na mataifa mbalimbali kukuza uchumi wa nchi. Tanzania ni miongoni mwa mataifa hayo ikiwa na utajiri wa vivutio vya utalii na maliasili.Tanzania ina aina mbalimbali za utalii na vivutio vyake kama vile hifadhi za Taifa, mbuga za wanyama, fukwe, sehemu za kihistoria, malikale na misitu.

Utalii wa misitu ni miongoni mwa maeneo muhimu na yanayokuwa kwa kasi Tanzania na duniani kwa ujumla. Huu ndiyo utalii daraja la kwanza katika viwango vya Shirika la Utalii Duniani (WTO).

Kwa Tanzania hifadhi za misitu ni eneo mojawapo lenye vivutio vya utalii vinavyotumika kwa ajili ya utalii ikolojia, utafiti, burudani za kutembea, kuendesha baiskeli, na mapumziko. Hifadhi hizi pia ni sehemu muhimu katika kuongeza makusanyo ya maduhuli ya Serikali katika jitihada za kuendeleza utalii kwenye maeneo ya misitu, ambapo mapato yanayotokana na viingilio kwenye hifadhi hizi yamekuwa yakiongezeka kila mwaka.

Aidha, usimamizi wa rasilimali za malikale na maeneo ya misitu yenye vivutio vya utamaduni, unaongeza mchango katika kufikia malengo ya Serikali ya kuwa na watalii milioni tano na mapato ya dola bilioni sita kwa mwaka ifikapo 2025.

Utalii huu kwa Tanzania unasimamiwa na kuendeshwa na Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS), ambapo kama wadau wa sekta ya utalii, wanaamini uhifadhi wa misitu ni muhimu katika kupeleka gurudumu la maendeleo ya utalii.

TFS unasimamia misitu ya hifadhi za mazingira asilia 20, yenye jumla ya eneo la takribani hekta 924,876.22. Kupandishwa hadhi kwa msitu kuwa hifadhi za mazingira asilia (nature forest Reserves) ni hadhi ya juu kabisa inayotambuliwa na shirika la kimataifa la uhifadhi (International Union of Conservation for Nature (IUCN), hivyo kuna jumla ya hifadhi 20 za mazingira asilia kutoka hifadhi 12 zilizokuwa na jumla ya hekta 305,600 mwaka 2015.

Hifadhi za mazingira asilia zimetengeneza mtandao mpana wenye fursa nyingi za kukuza utalii wa ndani na kwa wageni kutoka ndani na nje.

Recent News

  • TFS yapiga hatua kubwa katika uhifadhi wa misitu, ukuzaji utalii Tanzania Nov 06, 2021
  • Hifadhi ya Mji Mkongwe na Kaole ziboreshwe Nov 04, 2021
  • Miongozo wa namna ya kuvuna mikoko maeneo ya delta kukamilika mwezi huu Jul 19, 2021

Facebook

Ecotourism Destinations

The Forest Nature Reserve (NFR)

The Forest Nature Reserve (NFR) category of protected area (PA) offers the highest level of protection under the National Forest Act of Tanzania. FNRs are state-owned and are managed by the Tanzania Forest Services (TFS) Agency.

Read More

 

  • Overview
  • Mission and Vission
  • Climate Conditions
  • Terms and Conditions
  • Contact Details
  • Fees and Charges
  • Publications
  • Bronchures
  • Climate
  • Security
  • Geography
  • Ethnic Groups
  • Language
  • FAQ
  • Visa Application
Copyright © 2022 Tanzania Forest Services Agency. All Rights Reserved
  • Home
  • Feedback and Enquiry
  • Staff Mails